John 14:1-6
Isa Awatia Moyo Wanafunzi Wake
1 aIsa akawaambia, “Msifadhaike mioyoni mwenu, mnamwamini Mungu, niaminini na mimi pia. 2 bNyumbani kwa Baba yangu kuna makao mengi. Kama sivyo, ningeliwaambia. Naenda kuwaandalia makao. 3 cNami nikienda na kuwaandalia makao, nitarudi tena na kuwachukua mkae pamoja nami, ili mahali nilipo, nanyi mpate kuwepo. 4Ninyi mnajua njia ya kufika ninakokwenda.”Isa Ndiye Njia Ya Kwenda Kwa Baba
5 dTomaso akamwambia, “Bwana, sisi hatujui unakokwenda, tutaijuaje njia?” 6 eIsa akawaambia, “Mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu hawezi kuja kwa Baba isipokuwa kwa kupitia kwangu.
Copyright information for
SwhKC